Forest Industries Training Institute - FITI

Forest Industries Training Institute - FITI We offer Technician certificate in Forest Industries Technology and various short courses including

KATIBU MKUU WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI ATEMBELEA BANDA LA CHUO CHA VIWANDA VYA MISITU NANENANE 2026Katibu Mkuu wa Wizara ...
02/08/2026

KATIBU MKUU WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI ATEMBELEA BANDA LA CHUO CHA VIWANDA VYA MISITU NANENANE 2026

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes Kisaka Meena, leo tarehe 02 Agosti 2026, ametembelea banda la Chuo cha Viwanda vya Misitu (FITI) katika Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo (Nanenane) yanayoendelea katika viwanja vya Nzuguni, jijini Dodoma.

Katika ziara hiyo, Bi. Meena alipata fursa ya kufahamu shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na chuo, ikiwemo utoaji wa mafunzo ya uhifadhi wa misitu, usimamizi endelevu wa rasilimali za misitu, pamoja na teknolojia za uchakataji na uongezaji thamani wa mazao ya misitu.

Aidha, alipata nafasi ya kujionea bidhaa mbalimbali zinazotengenezwa na chuo kutokana na mazao ya misitu na kusisitiza umuhimu wa kuendelea kuimarisha elimu na ujuzi unaochangia matumizi endelevu ya rasilimali za misitu kwa maendeleo ya taifa.

FITI YAPOKEA UJUMBE KUTOKA WAGENINGEN UNIVERSITY & RESEARCH (WUR), UHOLANZIMkuu wa Chuo cha Viwanda vya Misitu (FITI), D...
25/07/2026

FITI YAPOKEA UJUMBE KUTOKA WAGENINGEN UNIVERSITY & RESEARCH (WUR), UHOLANZI

Mkuu wa Chuo cha Viwanda vya Misitu (FITI), Dkt. Zacharia Lupala, leo amepokea ujumbe kutoka Wageningen University & Research (WUR) ya nchini Uholanzi, uliowasili kupitia Dr. Nicholaus Memorial Nature Conservation, mmoja wa wadau muhimu wa Chuo katika utekelezaji wa Mafunzo kwa Vitendo (Field Practical Training - FPT) kwa wanafunzi.

Ushirikiano huo umejikita katika maeneo ya uhifadhi wa misitu, utunzaji wa mazingira na upandaji miti, ukiwa na lengo la kuwajengea wanafunzi ujuzi wa vitendo unaokidhi mahitaji ya sekta ya misitu.

Katika kikao kilichofanyika chuoni, pande zote zilijadili namna ya kuimarisha na kupanua ushirikiano uliopo kwa kubadilishana uzoefu na ujuzi katika sekta ya misitu, kuendeleza tafiti za pamoja, pamoja na kuboresha mafunzo ya kitaaluma na ya vitendo.

Ziara hiyo ni sehemu ya juhudi za Chuo cha Viwanda vya Misitu za kuendelea kujenga ushirikiano na taasisi za kimataifa ili kuimarisha ubora wa elimu, tafiti na maendeleo endelevu ya sekta ya misitu nchini.

DKT. LUPALA AWASHUKURU WATUMISHI WA FITI KWA USHIRIKIANO WAO.Mkuu wa Chuo Cha Viwanda vya Misitu (FITI), Dkt. Zacharia L...
24/07/2026

DKT. LUPALA AWASHUKURU WATUMISHI WA FITI KWA USHIRIKIANO WAO.

Mkuu wa Chuo Cha Viwanda vya Misitu (FITI), Dkt. Zacharia Lupala, amewashukuru watumishi wa chuo hicho kwa ushirikiano mkubwa wanaouonyesha katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku kwa ufanisi, jambo linalochangia maendeleo ya chuo na maslahi mapana ya Taifa.

Shukrani hizo amezitoa leo, tarehe 24 Julai 2026, wakati wa kikao cha watumishi wote kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chuo Cha Viwanda vya Misitu.

Akizungumza katika kikao hicho, Dkt. Lupala amesema FITI ina wajibu mkubwa wa kuhakikisha inatoa suluhisho la changamoto mbalimbali zinazoikabili nchi kupitia mafunzo bora, utafiti na ubunifu.

"Sisi k**a taasisi ya elimu tunalo jukumu kubwa la kuhakikisha tunatoa mafunzo yatakayowajengea wanafunzi wetu uwezo wa kujibu changamoto za soko la ajira. Ni muhimu kuwafundisha namna ya kutenda, kubuni na kuzalisha ili waweze kujiajiri na kuajiri wengine," amesema Dkt. Lupala.

Aidha, amewahimiza watumishi kuendelea kushirikiana, kufanya kazi kwa weledi na ubunifu ili kuimarisha ubora wa mafunzo na kuongeza mchango wa chuo katika maendeleo ya sekta ya misitu na uchumi wa Taifa.

Chuo Cha Viwanda vya Misitu kinatoa mafunzo ya Teknolojia ya Viwanda vya Misitu katika ngazi za Astashahada ya Awali, Astashahada na Stashahada. Dirisha la kutuma maombi ya kujiunga na chuo kwa mwaka wa masomo unaofuata bado liko wazi. Waombaji wanahimizwa kutuma maombi yao sasa na kuchangamkia fursa ya kupata elimu yenye kuzingatia ujuzi na mahitaji ya soko la ajira.

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania (TAFORI) Dkt. Revocatus Mushumbusi Leo Tarehe 13 Julai 2026 ame...
13/07/2026

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania (TAFORI) Dkt. Revocatus Mushumbusi Leo Tarehe 13 Julai 2026 ametembelea Banda la Chuo Cha Viwanda vya Misitu lililopo katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) na kukipongeza Chuo Cha Viwanda vya Misitu kwa Kushiriki katika Maonesho hayo ya 50 ya Biashara.

KAIMU MKURUGENZI WA IDARA YA MISITU NA NYUKI ATEMBELEA BANDA LA CHUO CHA VIWANDA VYA MISITU SABASABAKaimu Mkurugenzi wa ...
12/07/2026

KAIMU MKURUGENZI WA IDARA YA MISITU NA NYUKI ATEMBELEA BANDA LA CHUO CHA VIWANDA VYA MISITU SABASABA

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii, Bw. Daniel Pancrasi, leo tarehe 12 Julai 2026 ametembelea banda la Chuo cha Viwanda vya Misitu (FITI) katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba).

Akiwa katika banda hilo, Bw. Pancrasi alipata fursa ya kujionea bidhaa mbalimbali zinazotokana na mazao ya misitu zinazozalishwa na kutengenezwa na Chuo cha Viwanda vya Misitu Moshi. Bidhaa hizo zinaonesha ubunifu, ujuzi wa kitaalamu na mchango wa chuo katika kuongeza thamani ya mazao ya misitu pamoja na kuendeleza viwanda vinavyotegemea rasilimali za misitu.

Ziara hiyo pia ilitoa nafasi ya kujifunza kuhusu kozi mbalimbali zinazotolewa na chuo, teknolojia zinazotumika katika uchakataji wa mazao ya misitu, pamoja na fursa za mafunzo na ajira zinazopatikana kupitia sekta ya misitu.

Chuo cha Viwanda vya Misitu kinaendelea kutumia Maonesho ya Sabasaba k**a jukwaa la kutoa elimu kwa umma kuhusu matumizi endelevu ya rasilimali za misitu, kuongeza thamani ya mazao ya misitu na kuhamasisha vijana kujiunga na mafunzo ya ufundi yanayochangia maendeleo ya uchumi wa taifa.

Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Misitu Tanzania (TaFF), Dkt. Tuli Salumu Msuya, leo tarehe 03 Julai 2026, ametembelea banda la...
04/07/2026

Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Misitu Tanzania (TaFF), Dkt. Tuli Salumu Msuya, leo tarehe 03 Julai 2026, ametembelea banda la Chuo cha Viwanda vya Misitu (FITI) katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) yanayoendelea katika Viwanja vya Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.

Akiwa katika banda hilo, Dkt. Msuya alipata fursa ya kujionea shughuli mbalimbali za mafunzo, bidhaa na ubunifu wa wanafunzi pamoja na huduma zinazotolewa na chuo katika kuendeleza sekta ya viwanda vya misitu nchini.

Chuo cha Viwanda vya Misitu kilitoa shukrani kwa Mfuko wa Misitu Tanzania (TaFF) kwa mchango wake mkubwa katika kuboresha miundombinu ya kutolea mafunzo chuoni. Mchango huo umewezesha kukamilika kwa ujenzi wa jengo la Maabara ya Mbao pamoja na ununuzi wa vifaa vya kisasa vya maabara, hatua iliyoongeza ubora wa mazingira ya kujifunzia na kufundishia.

Aidha, TaFF inaendelea kufadhili ujenzi wa bweni la wasichana chuoni, mradi unaotekelezwa kwa lengo la kuboresha ustawi wa wanafunzi na kuongeza fursa za kupata elimu katika mazingira salama na rafiki.

Chuo cha Viwanda vya Misitu kinatoa pongezi na shukrani kwa TaFF kwa ushirikiano wake endelevu katika kuimarisha elimu ya ufundi na maendeleo ya sekta ya misitu nchini.

TEMBELEA BANDA LA CHUO CHA VIWANDA VYA MISITU LILILOPO KATIKA VIWANJA VYA SABASABA JIJINI DAR ES SALAAM NDANI YA BANDA L...
02/07/2026

TEMBELEA BANDA LA CHUO CHA VIWANDA VYA MISITU LILILOPO KATIKA VIWANJA VYA SABASABA JIJINI DAR ES SALAAM NDANI YA BANDA LA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII.

KUMBUKA

DIRISHA LA UDAHILI LIPO WAZI – CHUO CHA VIWANDA VYA MISITU (FITI)

Chuo cha Viwanda vya Misitu (FITI) kinapenda kuutaarifu umma kuwa dirisha la udahili kwa ngazi ya Astashahada na Stashahada (Diploma) ya Teknolojia ya Viwanda vya Misitu limefunguliwa rasmi kuanzia tarehe 28 Mei hadi 10 Julai 2026.

Sifa za Mwombaji

Mwombaji awe amehitimu kidato cha nne na kuwa na angalau ufaulu wa alama D nne (4), ambapo mbili (2) kati ya hizo ziwe za masomo ya sayansi. Wanafunzi wanapata mafunzo kwa vitendo kupitia mitambo, maabara na karakana za kisasa.

Kumbuka kuwa wanafunzi wa chuo chetu wanapatiwa mikopo na Serikali kupitia Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB). Hivyo basi, unapofanya maombi ya kujiunga na chuo, kumbuka pia kuomba mkopo kupitia HESLB.

Karibu FITI upate taaluma na ujuzi wa uhifadhi wa misitu na matumizi endelevu ya mazao ya misitu.

Huduma za Hosteli

Hosteli zipo za kutosha kwa wanafunzi.

Mawasiliano

+255 786 704 784 – Afisa Udahili

+255 757 182 141 – Msajili wa Wanafunzi

+255 627 906 206 – Afisa Masoko

Barua Pepe

[email protected]

[email protected]

DIRISHA LA UDAHILI LIPO WAZI – CHUO CHA VIWANDA VYA MISITU (FITI)Chuo cha Viwanda vya Misitu (FITI) kinapenda kuutaarifu...
24/06/2026

DIRISHA LA UDAHILI LIPO WAZI – CHUO CHA VIWANDA VYA MISITU (FITI)

Chuo cha Viwanda vya Misitu (FITI) kinapenda kuutaarifu umma kuwa dirisha la udahili kwa ngazi ya Astashahada na Stashahada (Diploma) ya Teknolojia ya Viwanda vya Misitu limefunguliwa rasmi kuanzia tarehe 28 Mei hadi 10 Julai 2026.

Sifa za Mwombaji

Mwombaji awe amehitimu kidato cha nne na kuwa na angalau ufaulu wa alama D nne (4), ambapo mbili (2) kati ya hizo ziwe za masomo ya sayansi. Wanafunzi wanapata mafunzo kwa vitendo kupitia mitambo, maabara na karakana za kisasa.

Kumbuka kuwa wanafunzi wa chuo chetu wanapatiwa mikopo na Serikali kupitia Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB). Hivyo basi, unapofanya maombi ya kujiunga na chuo, kumbuka pia kuomba mkopo kupitia HESLB.

Karibu FITI upate taaluma na ujuzi wa uhifadhi wa misitu na matumizi endelevu ya mazao ya misitu.

Huduma za Hosteli

Hosteli zipo za kutosha kwa wanafunzi.

Mawasiliano

+255 786 704 784 – Afisa Udahili

+255 757 182 141 – Msajili wa Wanafunzi

+255 627 906 206 – Afisa Masoko

Barua Pepe

[email protected]

[email protected]

Dirisha la maombi ya mikopo Mwaka wa Masomo 2026/2027 limefunguliwa.
21/06/2026

Dirisha la maombi ya mikopo Mwaka wa Masomo 2026/2027 limefunguliwa.

19/06/2026

Washiriki wa mafunzo ya mbinu za kuzuia, kupambana na kuzima moto wa misituni wamekipongeza Chuo cha Viwanda vya Misitu (FITI) kwa kuandaa mafunzo yenye ubora wa hali ya juu, yaliyowezesha kujifunza kwa vitendo na kubadilishana uzoefu.

Wamesema mafunzo hayo yamewajengea uwezo wa kutumia mbinu salama na za kisasa katika kukabiliana na moto wa misituni, na wameeleza matarajio yao ya kuyatumia maarifa hayo kulinda misitu, mazingira na rasilimali za taifa.

FITI inaendelea kuwa kitovu cha utoaji wa mafunzo ya kitaalamu yanayojenga uwezo kwa maendeleo endelevu ya sekta ya misitu.

Address

Forest Industries Training Institute, Box 1925
Moshi

Opening Hours

Monday 07:30 - 15:30
Tuesday 07:30 - 15:30
Wednesday 07:30 - 15:30
Thursday 07:30 - 15:30
Friday 07:30 - 15:30

Telephone

+255787676981

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Forest Industries Training Institute - FITI posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Forest Industries Training Institute - FITI:

Shortcuts

Share

Category